Posts

Showing posts from January, 2017

Gazeti la Mwanahalisi laomba radhi rasmi.

Image
Baada ya kupewa siku kadhaa na serikali ya kuomba hatimaye kampuni ya Halihalisi inayochapisha gazeti la Mwanahalisi wameomba radhi rasmi kwa Rais

Donald Trump amfukuza kazi mwanasheria mkuu wa Marekani.

Image
Dakika 27 zilizopita Mshirikishe mwenzako Image caption Kaimu mwanasheria mkuu wa Marekani Sally Yates Rais wa Marekani Donald Trump amemfuta kazi kaimu mwanasheria mkuu Sally Yates saa chache tu baada ya kuwaagiza mawakili wa idara ya haki nchini humo kutotetea uamuzi wa kuwawekea vikwazo raia wanaotoka katika baadhi ya mataifa ya kiislamu. Taarifa ya Ikulu ya Whitehouse imemshtumu kwa usaliti. Sally Yates ambaye aliteuliwa na Obama alisema kuwa hafikirii kwamba marufuku hiyo ya muda kwa raia wa mataifa saba ya Kiislamu ni halali. Trump: Wakimbizi wa Syria hawaruhusiwi Marekani Trump ajitetea kuhusu sera ya usafiri Sudan yapinga amri ya Trump Amri ya Trump: Ni nani anaathirika? Wadhfa wake umechukuliwa na kiongozi wa mashtaka katika mahakama ya kijimbo huko Virginia Dana Boente. Agizo hilo la rais lililotiwa saini Ijumaa iliopita limesababisha maandamano nchini Marekani na ughaibuni. Awali kundi moja la wanadiplomasia liliandika barua likikosoa ag

Zaidi ya watu milioni moja wasaini barua kumzuia Trump kuzuru Uingereza

Image
Saa moja iliyopita Mshirikishe mwenzako Haki miliki ya picha PA Image caption Waziri Mkuu Teresa May alitangaza muwaliko huo wakati akiwa ziarani Marekani. Zaidi ya watu milioni moja wa Uingereza wamesaini barua ya kutoa shinikizo kwa serikali ya Uingereza kusitisha ziara rasmi iliopangwa baadaye mwaka huu ya rais Donald Trump. Barua hiyo iliyoandikwa kufuatia agizo la rais Trump dhidi ya wahamiaji, inaeleza kuwa kuja kwake kutamuaibisha Malkia Elizabeth. Idadi ya watu wanaoendelea kusaini kupinga Mwaliko wa Trump nchini Uingereza inaendelea kuongezeka, tangu Marekani kuweka vikwazo dhidi ya wageni hatua iliyozua ghadhabu kote duniani. Amri ya Trump: Ni nani anaathirika? Sudan yapinga amri ya Trump Amri ya Trump: Ni nani anaathirika? Waziri Mkuu Teresa May alitangaza muwaliko huo wakati akiwa ziarani Marekani. Afisi yake imesema japo haikubaliani na baadhi ya sera za Trump hata hivyo ni vyema Uingereza kuwa na ushirikiano wa karibu na Marekani. Kiong

GAZETI LA MWANAHALISI LAPEWA MASAA 24 WAOMBE RADHI.

Image

Google kuwarudisha wafanyikazi kufuatia agizo la Trump

Image
28 Januari 2017 Mshirikishe mwenzako Image caption Kampuni ya Google imewataka wafanyikazi wanaofanya kazi katika mataifa ya kigeni kurudi nchini Marekani kufuatia agizo la rais wa taifa hilo Donald Trump Kampuni ya Google imewataka wafanyikazi wanaofanya kazi katika mataifa ya kigeni kurudi nchini Marekani kufuatia agizo la rais wa taifa hilo Donald Trump kuwazuia raia wa mataifa sitaya Kiislamu kuingia nchini humo. Wahamiaji wa Syria wamepigwa marufuku kuingia nchini humo itakapotolewa ilani nyengine. Visa za raia wa mataifa sita ikiwemo Iran na Iraq hazitatolewa kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo. Googole imeambia BBC ina wasiwasi kuhusu agizo hilo na mikakati ambayo huenda ikawazuia watu wenye vipaji kuingia nchini Marekani. Trump kuwazuia wahamiaji kuingia Marekani Donald Trump kuwarejesha wahamiaji kwao Wahamiaji New York wana hofu kuhusu Trump Marekani kujenga ukuta mara moja Mwandishi wa BBC aneyesimamia maswala ya kibiashara Joe Lyam anasema

MKUU WA MAGEREZA GAMBIA AKAMATWA WAKATI AKIJARIBU KUTOROKA .

Image
Jeshi la Polisi nchini Senegal limemkamata mkuu wa magereza nchini Gambia, Jenerali Bora Colley akijaribu kutoroka kuelekea Guinea Bissau. Jenerali Bora Colley alikamatwa siku ya Jumatano na baadaye kukabidhiwa jeshi la Senegal, taarifa hizo zikitolewa na jeshi la Polisi. Aidha, Watu wa haki za kibinaadamu Gambia wamesema kuwa kiwango kikubwa cha ukandamizi kilifanywa chini ya uongozi wa aliyekuwa rais wa taifa hilo, Yahya Jammeh ikiwemo mateso pamoja na mauaji ya kiholela ambayo yalifanyika katika jela.

RAIS MAGUFURI HARIDHIA MKUU WA WILAYA YA UYUI KUJITUMBUA.

Image

Kiongozi wa Mexico akataa kulipia gharama za ujenzi wa ukuta

Image
Rais wa Mexico anafikiria kufutilia mbali ziara aliyoipanga kuifanya Washington wiki ijayo kufuatia amri ya Rais Donald Trump kuwa ujenzi wa ukuta kati ya nchi hizo mbili uanze mara moja, amesema msemaji wa ngazi ya juu. Katika hotuba yake kwa njia ya televisheni kwa taifa Jumatano, Rais Enrique Pena Nieto amesema anasikitishwa na hakubaliani na uamuzi wa Marekani, na amerejea tena kusema  kwamba Mexico haitolipa gharama za ujenzi wa ukuta huo pamoja na Trump kutoa kauli hiyo. “Mexico haiamini katika kuweka ukuta, “alisema rais huyo. “Nimesema mara nyingi, Mexico haitalipa gharama zozote za ujenzi wa ukuta.” Pena Nieto hakusema moja kwa moja kuhusu safari yake, lakini akagusia kuwa atangojea ripoti kutoka kwa maafisa wa ngazi ya juu wa Mexico ambao hivi sasa wanakutana na uongozi wa Trump huko Washington.

MKUU WA WILAYA UYUI HAJIUZURU...

Image
Mkuu wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, Gabriel Simon Mnyele  amejiuzulu nafasi hiyo leo Alhamisi Januari 26, 2017 na kuwaaga madiwani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano alioufanya wilayani humo. Akieleza sababu ya kufanya uamuzi huo, Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa alimwandikia Rais Dkt Magufuli barua ya kujiuzulu nafasi hiyo akielezea kusongwa na majukumu binafsi. Mkuu wa Wilaya, Gabriel Simon Mnyele alikuwa miongoni mwa Wakuu wa Wilaya 139 walioteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 26 Juni, 2016. Bw.Gabriel Mnyele hakuwa tayari kuelezea maamuzi aliyochukua na kuwataka Waandishi waliokuwa wakihoji hatua ya maamuzi yake wasubiri tamko kutoka juu. "Mimi sina la kusema kuhusu hilo nimeamua mwenyewe, kwani mmesikia kuwa nimetumbuliwa?"  Aliwahoji waandishi.

TFF YATUPILIA MBALI RUFAA YA KLABU YA POLISI DAR DHIDI YA SIMBA BAADA YA KUMCHEZESHA MCHEZAJI WAKE LUFUNGA

Image
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limepokea rufaa kutoka Klabu ya Polisi Dar es Salaam dhidi ya Klabu ya Simba kuhusu kumchezesha Mchezaji Novalty Lufunga katika mchezo wao wa Raundi ya Tano ya Kombe la Azam Sports Federation Cup 2017. Madai ya Polisi ni kwamba Mchezaji Novalty Lufunga alioneshwa kadi nyekundu kwenye Simba dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa Azam Sports Federation Cup 2015/2016 uliofanyika Uwanja wa Uhuru, Januari 22, mwaka huu. Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetupilia mbali rufaa hiyo kwa kukosa vigezo vya kikanuni katika uwasilishaji wake na hivyo kukosa sifa ya kusikilizwa. Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 18 (1) na (2) ya Kanuni za Kombe la Shirikisho la Azam Sports HD. Kanuni ya 18 (1) inasema: “Malalamiko yoyote kuhusiana na mchezo yawasilishwe kwa maandishi kwa kamishna wa mchezo au TFF sio zaidi ya masaa sabini na mbili (72hrs) baada ya kumalizika mchezo.” Kanuni ya 18 (2) inasema: Ada ya malalamiko ni shilingi laki tatu

Rasmi: Ulimwengu asaini miaka mitatu sweden..

Image
Ulimwengu akiwa mazoezini Sweden. Klabu ya AFC Eskilstuna ya Ligi Kuu Sweden imethibitisha kuingia mkataba wa miaka mitatu na mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Ulimwengu. Kupitia mtandao wa klabu hio, Ulimwengu ataichezea Eskilstuna kwa misimu mitatu baada ya kumwaga wino leo. Ulimwengu amejiunga na timu hiyo kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake wa miaka mitano na mabingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika, TP Mazembe.

NASA launches unofficial Twitter account in defiance of Donald Trump

Image
You can count NASA as the third federal agency in the past twenty-four hours to defy Donald Trump by launching unofficial non-government Twitter accounts which Trump can’t control or sensor. First it was the National Park Service, which went rogue on Twitter after Trump forced deletions of factual tweets he didn’t like. Then the EPA went rogue earlier today. And now NASA has launched its own rogue Twitter account in order to make sure its truths are heard against Trump’s will. If only Trump would leave earth. The rogue Twitter account in question, which is literally called @RogueNASA, has only existed for five hours and has already gained a significant popular following. It started off by tweeting “We cannot allow Mr. Trump to silence the scientific community. We need peer-reviewed, evidence-based research MORE THAN EVER now,” while adding “How sad is it that government employees have to create rogue Twitter accounts just to communicate FACTS to the American public?” The account

NEW FEATURE: From February 5 Onwards, WhatsApp Will Let You Know When Someone Screenshots Your Chat

Image
BY   MANDISA NDABA   ·   JANUARY 26, 2017 Califo rnia  – Jan Koum, the CEO of WhatsApp,the biggest and cheapest messaging application has announced that the next upgrade of the application is going to include the option of being notified if someone screenshots your conversation. This upgrade comes after the majority of users requested the option, especially married couples and the elderly age according to him.“After all these years, we’ve reached the conclusion to add it”,he was quoted. “The functioning is simple, just like the blue tick.You will have the option activated by default. If it’s checked, you’ll be notified if someone screenshots your conversation, and others will be notified if you screenshot theirs. If it’s unchecked, no one gets notified”, stated Koum. A high number of users expressed disappointment in relation to this feature and an online poll is still ongoing to determine the more accurate figures. Source : iMzansi

Mwanamfalme anyongwa Kuwait

Image
Saa moja iliyopita Mshirikishe mwenzako Haki miliki ya picha AFP Image caption Serikali ya Kuwait imewanyonga wafungwa saba kwa mara ya kwanza tangu 2013 Serikali ya Kuwait imewanyonga wafungwa saba kwa mara ya kwanza tangu 2013, akiwemo mmoja wa jamaa ya familia ya kifalme. Walinyongwa katika jela ya Central kulingana na taarifa iliotolewa na kitengo cha habari cha serikali Kuna. Jamaa huyo kutoka familia ya kifalme alitajwa kuwa Faisal Abudallah Al Jaber Al Sabah ambaye alipatikana na hatia ya kupanga mauaji mbali na kumiliki silaha kinyume na sheria. Wafungwa wengine walionyongwa ni pamoja na raia wa Ufilipino, Misri, Ethiopia na Bangladesh. Walipatikana na hatia ya uhalifu ikiwemo mauaji, jaribio la mauaji ,utekaji nyara na ubakaji. Mwanamfalme aliyekiri kuua akatwa shingo Saudia Al Sabah alipatikana na hatia ya kumuua mwanamfalme mwengine mwaka 2010. Mwandishi wa BBC mashariki ya kati ambaye ni muhariri wa eneo hilo Sebastian Usher alisema ku

Wasomali 90 na Wakenya wawili watimuliwa Marekani

Image
Wasomali 90 na Wakenya wawili watimuliwa Marekani Dakika 5 zilizopita Mshirikishe mwenzako Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Rais wa Marekani Donald Trump Raia takriban 90 wa Somalia na wawili wa Kenya wametimuliwa kutoka Marekani saa chache baada ya taarifa kuibuka kwamba Rais Donald Trump atakabiliana na watu wanaoishi nchini humo kinyume cha sheria. Wote wamewasili katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi. Msemaji wa serikali ya Kenya Eric Kiraithe ameambia BBC kwamba raia hao wa Somalia watasafirishwa moja kwa moja hadi Mogadishu. Trump kuwazuia wahamiaji kuingia Marekani Bw Trump alisema Jumatano itakuwa siku muhimu kwa usalama wa Marekani. Anatarajiwa kuweka masharti makali kwa raia wa mataifa saba ya Mashariki ya Kati na Afrika yenye idadi kubwa ya Waislamu wanaotafuta viza za kwenda Marekani. Watakaoumia na watakaofaidi chini ya Trump Marekani Melania Trump kuchelewa kuingia White House